SHINDANO
  maalum lililotamba miaka nyuma la Maisha Plus, ambalo washiriki wake  
hukaa kwa miezi miwili kijijini, linatarajiwa kuanza hivi karibuni kwa  
kushirikiana na shirika la Oxfam Tanzania, kupitia program yake ya ‘Mama
  shujaa wa chakula’.
Akizungumza
  kwa jana, Kiongozi Mtendaji wa kampuni ya DMB, Masoud Ali ‘Masoud  
Kipanya’ alisema kuwa, shindano hilo la aina yake linakuja tena kwa  
msimu wa tatu, likiwa na utofauti kabisa, huku mambo mbalimbali  
yakiboreshwa, ikiwemo mshindi kuibuka na kitita cha sh milioni 20.
Kipanya
  alisema kuwa, kwa kushirikiana na wadhamini wakuu, Oxfam Tanzania,  
kupitia program yao ya ‘Mama shujaa wa chakula’, ambako watapata fursa  
ya kuwaweka wanawake kwenye shindano, kwa kukaa ndani ya jumba hilo la  
Maisha Plus huko kijijini kwa wiki mbili.
“Kwa
  kushirikiana na Oxfam, shindano hili tumeborsha na litakuwa la aina  
yake, ambapo washiriki watakaobahatika kushiriki, watafurahia na  
watajifunza mengi na safari hii Mama shujaa wa chakula nao watabahatika 
 kukaa kwa wiki mbili, kisha watatoka na washiriki wa Maisha Plus  
kuendelea na kinyang’anyiro cha kuwania kitita hicho cha milioni 20,”  
alisema Kipanya.
Aidha,
  aliwataka vijana wa kitanzania, kuchangamkia fursa hiyo, ambako  
wanatarajia kuanza kufanya usaili mkoani Arusha, Agosti 3 na kisha  
kuendelea kwenye mikoa mingine 14, ikiwemo ya Bara na viswani Zanzibar.
Pia,
  alitoa wito kwa wadhamini wengine, kutumia nafasi hii kujitokeza ili  
kupata kutangaza, kwani shindano hilo licha ya kufanyika misimu miwili  
ya 2009 na 2010,  huku 2011 likishindwa kufanyika kutokana na kukosa  
udhamini, limejizolea sifa na kupendwa na watu wa rika mbalimbali.
 Habari kwa hisani ya www.fatherkidevu.blogspot.com


 
 









 
 
 
 
