Thursday, May 31, 2012

MASTAA WASHINDANA KUANIKA MAPAJA YAO

                                                             Aunt Ezekiel.
                                                    Mayasa Mrisho ‘Maya’.
                                                     Jennifer Kyaka ‘Odama’.

Na Imelda Mtema

SURA za mauzo kwenye anga la Bongo Movies, Jennifer Kyaka ‘Odama’, Aunt Ezekiel na Mayasa Mrisho ‘Maya’ walifunikana kwa kuvaa nguo zenye kuacha mapaja yao nje hali iliyozua ‘muwashawasha’ kwa wanaume wenye tamaa za mahaba.
Ishu hiyo ilichukua nafasi juzikati kwenye Ukumbi wa Nyumbani Lounge, jijini Dar ambapo mastaa hao walialikwa kusherehekea uzinduzi wa bidhaa mpya ya kinywaji.
“Mh! Jamani hawa wametufanyia makusudi kushindana kuvaa viguo vifupi, hawajui kuwa wanatupa wakati mgumu?” alisikika akihoji mdau mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Dick.
Habari na www.globalpublisher.com

DUDE: ALIYEIROGA BONGO MOVIES AMEKUFA

                                                           Kulwa Kikumba ‘Dude’

Na Erick Evarist

MSANII Kulwa Kikumba ‘Dude’ ameweka ‘plain’ kuwa kitendo cha wasanii wenzake (Bongo Movies Club) kumtenga amekifananisha na tasnia hiyo ya filamu kurogwa na mtu ambaye ameshafariki.
Akifafanua kauli yake hiyo, Dude alisema wasanii wameshindwa kuelewa kuwa wanapaswa kukanyana wenyewe kwa wenyewe lakini anapofanya hivyo wanafikia hatua ya kumtenga.
“Tunashindwa kuitumia fursa ya rais wetu anayependa sanaa kwa sasa, badala yake tunafanya mambo ya ajabu ambayo kimsingi yanatudhalilisha kwa jamii.
“Hatujui rais ajaye atapenda nini, kama akipenda uvuvi si itakuwa imekula kwetu...sasa wasanii ukiwakumbusha wabadilike, wao wanakuona adui,” alisema Dude.
Hivi karibuni ilidaiwa kuwa Dude ametengwa na Club ya Bongo Movies baada ya staa huyo kufanya mahojiano na Kituo cha Runinga cha Clouds na kuwaonya wenzake juu ya mwenendo wa kitabia.

 www.globalpublisher.com

Tuesday, May 29, 2012

AJINYONGA KWA MADAI YA UGUMU WA MAISHA

Jamaa akiwa ananing’inia muda mchache baada ya kujinyonga.
Marehemu akionekana kwa nyuma.
Baada ya kuteremshwa chini na Wasamaria wema.
Mke wa marehemu akilia kwa uchungu.
Majirani waliokusanyika eneo la tukio.

MWANAMME mmoja ambaye hakutambulika jina lake, aliyekuwa mkazi wa Kigogo-Mbuyuni jijini Dar es Salaam asubuhi ya kuamkia leo (Mei 29), amejinyonga kwa madai ya ugumu wa maisha uliosababishwa na kukosa ajira.
Wakizungumza na mtandao wa huu, baadhi ya majirani ambao walihojiwa walisema kuwa jamaa huyo kwa muda mrefu alikuwa hana kazi hivyo kumsababishia ugumu wa maisha ambao ulikuja kumfanya ajinyonge.
“Siku zote mwanaume ameumbwa kutafuta riziki na si kukaa kusubiri kuletewa riziki. Jamaa huyu alikuwa akikaa tu nyumbani akimuachia mkewe aende akatafute riziki, matokeo yake ndio haya,” alisema jirani mmoja aliyekuwepo eneo la tukio.

Habari na www.globalpublisher.com
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...