Saturday, September 10, 2011

BILIONEA NAMBA MOJA AFRIKA BWANA ALIKO DANGOTE

http://www.jisikienyumbani.blogspot.com/


Tajiri namba moja barani Afrika kwa mwaka huu 2011 ni Bilionea wa Nigeria.Kwa mujibu wa majarida na mitandao mbalimbali dunia inamtambau kama tajiri wa kwanza barani Afrika na anashika nafasi ya 51 kwa utajiri duniani.Bwana Aliko Dangote raia wa Nigeria mwenye miaka 53 aliyepanda ghafta baada ya kuongezeaka utajiri wake kwa zaidi ya asilimia 20  na kufikia Dola 13.8 bilioni za kimarekani tokea mwaka jana alikua anashika nafasi ya saba kwa mabilionea wa Afrika.Bilionea huyu anayemiliki kampuni kadha nchini kwao ambazo ni Dangote Cement,Dangote Flour kama za Azam.,Dangote Sugar na Real estate

NI MSIBA WA KITAIFA MELI YA ZAMA ZANZIBAR.


Meli ya Spice iliyotoka kisiwani unguja kuelekea pemba katika bahari ya hindi imezama katika mkondo wa nungwi .Tukio hili limetokea usiku wa kuamkia leo.Inakadiriwa zaidi ya watu 610 mpaka 1000 walikuwamo katika meli hiyo kama abiria wakielekea pemba.Mamia ya watanzania wakiuzunika bara na visiwani Zanzibar kwa kuwapoteza ndugu,jamaa na marafiki zao katika tukio hili.Uko Zanzibar wananchi wengi wakiwa katika uzuni na harakati za kuwaokoa majerui zikiendelea kwani bahadhi ya majerui wameokolewa japo sio wengi lakini zoezi la uokoaji linaendelea.

Tuesday, September 6, 2011

Yobo afurahia kurudi klabu ya Fenarbahce

Mlinzi wa Everton Joseph Yobo amejiunga tena na klabu ya Uturuki ya Fenerbahce kwa mkopo wa muda mrefu

Mchezaji huyo wa timu ya taifa ya Nigeria mwenye umri wa miaka 31, msimu uliopita aliichezea klabu hiyo kwa mkopo, akaisaidia kuweza kunyakua ubingwa wa ligi ya Uturuki maarufu Super Lig.

Yobo, ambaye mkataba wake na Everton unamalizika mwaka 2014, hakucheza mechi yoyote ya maandalizi ya Ligi Kuu ya England.

"Nina furaha kila kitu kimekamilika, ilikuwa miezi mitatu migumu," alisema.

Fenerbahce ilikuwa na nia ya kuendelea kumtumia mlinzi na mkataba huo mpya wa mkopo ulikamilishwa kabla ya kumalizika dirisha la usajili nchini Uturuki siku ya Jumatatu.

Yobo alionekana tayari kujiunga na klabu ya Fenerbahce mwishoni mwa msimu wa 2010-11 lakini badala yake akarejea Everton.

Tangu wakati huo klabu hiyo ya Uturuki ilikuwa katika kashfa ya kupanga matokeo ya mechi na ikapoteza ubingwa wa ligi na kufuzu kwa ubingwa wa Europe.

Lakini Yobo hayupo tayari kujumuishwa na kashfa hiyo.

Fenerbahce pia imekamilisha uhamisho wa mshambuliaji kutoka Cameroon Henri Bienvenu Ntsama kutoka klabu ya BSC Young Boys ya Switzerland.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 23 ametia saini mkataba wa miaka minne kuichezea klabu hiyo wenye thamani ya dola milioni 5.7.

Saratani 'yamwuua Mugabe'

Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe ana saratani ya kibofu iliyoenea kwenye viungo vengine, kulingana na nyaraka za kidiplomasia za Marekani zilizofichuliwa.

Nyaraka hiyo, iliyochapishwa na mfichua siri Wikileaks, inamtaja gavana wa benki kuu Gideon Gono akisema daktari wa Mugabe amemsihi aachie madaraka.

Nyaraka hiyo, iliyoandikwa mwaka 2008 na ubalozi wa Marekani mjini Harare, pia inasema Bw Mugabe mwenye umri wa miaka 87 anaweza kufariki dunia ifikapo mwaka 2013.
Bw Gono, mshirika mwaminifu wa Bw Mugabe, amepuuzilia mbali nyaraka hizo akisema ni "taarifa za kubuni".

Nyaraka hizo zinamnukuu Bw Gono akisema saratani hiyo "imesambaa na, kulingana na madaktari, itasababisha kifo chake katika kipindi cha miaka mitatu mpaka mitano."

Katika mahojiano na shirika la habari la Reuters Septemba mwaka jana, Bw Mugabe- aliyekuwa madarakani tangu mwaka 1980- alipinga uvumi kuwa alikuwa akifa kutokana na saratani na alipooza.

Ciara And Ludacris Rumoured To Be Dating!They have dated in past, so is it back on?

R&B Singer Ciara and rapper Ludacris are rumoured to be dating.

According to MediaTakeout.com, the two have been getting very close recently and say that the pair actually dated for a while back in the day but called it quits.

Ciara was spotted at Ludacris’ side for two days straight during “Luda Weekend” in Atlanta. His current girlfriend Eudoxie was not spotted until the ‘Goodies’ star was out of town

A source told the site: “Ciara asked that Luda NOT bring [Eudoxie] to [club] Opera. And the two were kickin’ it all night together. Of course, they left together too.” Luda and CiCi were also out the next morning to pose for pictures which have been posted online.

When Eudoxie and the 33-year-old MC were later reunited, onlookers described some discord between the pair
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...