Saturday, February 23, 2013

Polisi yatangaza dau aliyemuua Padri Mushi

WAKATI kukiwa na taarifa kwamba maofisa wa Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI) wametua nchini kwa ajili ya kufanya upelelezi wa mauaji ya Padri Evarist Mushi, Jeshi la Polisi limetangaza dau la Sh10 milioni kwa atakayefichua aliyemuua padri huyo.
Padri Mushi aliuawa kwa kupigwa risasi Jumapili iliyopita wakati akienda kuongoza ibada katika Kanisa la Mtakatifu Teresia lililopo Beit el Ras nje kidogo ya mji wa Zanzibar, ambapo inadaiwa kuwa waliomuua walikuwa wamepanda pikipiki aina ya Vespa na walimfyatulia padri huyo risasi tatu akiwa ndani la gari yake.
Wakati polisi wakitangaza dau hilo, Sheikh Ali Khamis Ali (65) mkazi wa Kitope Kaskazini Unguja, aliuawa jana kwa kukatwa mapanga mjini Zanzibar, baada ya wezi kuvamia shambani kwake.
Habari za kuaminika zilizopatikana juzi zinaeleza kuwa maofisa hao wa FBI, wako nchini na tayari na wamekutana na baadhi ya viongozi wa Serikali kwa ajili ya kuanza kazi hiyo.
Chanzo chetu cha habari kimeeleza kuwa maofisa hao walikutana na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi kwa ajili ya kuangalia ni namna gani watafanya shughuli zao katika upelelezi huo.
Pamoja na ushiriki FBI, taarifa zinaeleza kuwa maofisa wa Serikali ya Tanzania wamezungumza na taasisi za upelelezi za nchi tano, ili kuongeza nguvu katika upelelezi huo.
Taasisi nyingine inayotajwa kuwa huenda ikashiriki katika uchunguzi huo ni Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai ya Uingereza (Scotland Yard).
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Ame Silima alilithibitishia gazeti hili kwamba Serikali imeanza kufanya mazungumzo na mashirika mbalimbali ya upelelezi duniani kwa ajili ya kushirikiana nayo kuchunguza mauaji ya Padri Mushi, lakini akasema kuwa ni mapema mno kuyataja.
“Tumefuata maagizo aliyotoa Rais Kikwete kwamba tushirikishe mataifa mbalimbali kuchunguza mauaji yaliyotokea Zanzibar, siwezi kutaja kwa majina, ila tayari tumeanza kuzungumza na nchi mbalimbali,” alisema Silima.
Akizungumza mjini Zanzibar jana, Kamishna wa Polisi visiwani humo, Mussa Ali Mussa alisema kuwa hadi sasa hakuna mtu aliyefikishwa mahakamani kuhusiana na tukio hilo la mauaji.
“Hakuna aliyefikishwa mahakamani, lakini wapo watu ambao wamekamatwa wakihusishwa na tukio hili na tunaendelea kuwahoji, wengine tunawaachia,” alisema na kuongeza:
“Tumeahidi kutoa Sh10 milioni kwa mtu yeyote, atakayetoa taarifa za mauaji ya Padri Mushi, hii itakuwa kama zawadi tu.”

Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa maofisa wa FBI wamekutana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Said Mwema kuzungumzia suala hilo la mauaji ya Padri Mushi.
Tukio hili la kuuawa kwa Padri Mushi linahusishwa na matukio kadhaa ya vurugu zilizoambatana na uchomaji moto makanisa na mali mbalimbali hivi karibuni.
Moja ya matukio hayo ni lile la Jumatano ya Desemba 25 mwaka jana ambapo Padri wa Kanisa Katoliki lililopo Mpendae visiwani Zanzibar, Ambrose Mkenda, alijeruhiwa kwa risasi na watu wasiojulikana nje ya nyumba yake, saa 12 jioni wakati akitoka kanisani.
Padri huyo alipatiwa matibabu katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja na baadaye alihamishiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu zaidi.
Wakati huo huo, Sheikh Mussa Ali Mussa ambaye alikuwa kiongozi wa Misikiti ya Kitope na Mwakaje ameuawa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja, Ahmada Khamis alisema kuwa kiongozi huyo, aliuawa kutokana na kipigo alichokipata kutoka kwa wezi waliovamia shamba lake.
Kuuawa kwa Sheikh huyo kumezua hofu kwa wakazi wa Zanzibar wakidhani ni kitendo cha kulipiza kisasi, lakini Polisi imetuliza hali hiyo kwa kusema kwamba aliuawa na wezi waliokuwa wakiiba shambani kwake.
Alisema kwamba baada ya kuwafuma wezi hao wakiiba shambani kwake walimshambulia kwa mapanga na kupoteza uhai wake na kwamba hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo.

Habari imeandikwa kwenye mwananchi.co.tz

Download [AUDIO] | Dully Sykes-Funga Domo Lako


Thursday, February 21, 2013

Q-Chief akimjibu Diamond, muziki wake mpya na show yake ijayo


Sijui wakati anajibu hayo maswali alikuwa kwenye hali gani, sijui alikuwa amekasirika, sijui alikuwa out of mood sijui alikuwa okay, lakini all in all najua kila mtu ana uhuru wa kuongea kile anachojisikia na hajawekea mipaka, as long as kinamsatisfy yeye na kinawafurahisha wengine kwenye umma - Q-Chief.

PICHA 3: LEBEL MPYA YA MAVAZI YA RAPPER BIG SEAN

Rapper BIG Sean wa Good Music anatarajiwa Kuzindua Clothing Line Mpya Mwezi Huu Itwayo Aura Gold. Rapper Huyo Kutoka Detroit anatoa Nguo hizo Kupitia Aura Gold nazitaitwa "Finally Famous" Mjini Las Vegas Week Hii .Mpaka sasa report zinasema "Finally Famous" Itakuwa na Nguo Kama T-shirts, Kofia ,Nguo Za Ndani, Masweta na Makoti.Kwenye Jarida La Vide Toleo La  February/March 2013 utaona baadhi ya Nguo hizo. Mwaka jana Big Sean alishirikiana na  Adidas na kutengeneza viatu vya Finally Famous na kwa sasa Fahamu kuwa Album Mpya ya Big Sean Inatoka Mwaka Huu Na Mpaka sasa ametoa taarifa kuwa itaitwa  Hall Of Fame:Memoirs Of A Detroit Player. 




Matokeo Kidato cha Nne 2012 ni FEKI (yamepikwa) - GREEN ACRES

Matokeo kidato cha nne ‘feki’

• Mkurugenzi Green Acres afichua siri nzito



WAKATI mjadala wa matokeo mabaya ya kidato cha nne ukiendelea kulitikisa taifa, kashfa mpya ya matokeo hayo imeibuliwa.

Kashfa hiyo mpya imeibuliwa na Mkurugenzi wa Shule ya Green Acres, Julian Bujugo, kwamba matokeo ya baadhi ya shule nchini ikiwamo yake yamechakachuliwa.

Akizungumza na gazeti hili jana, Bujugo alisema kuwa baadhi ya wanafunzi kwenye shule yake hawakufanya mitihani ya kidato cha nne, lakini matokeo yanaonesha wamefaulu kwa kupata alama za juu.

Alitaja mfano wa mwanafunzi, Humphrey Sanga, mwenye namba 01197/148, ambaye hakufanya mitihani hiyo lakini matokeo yanaonesha amefaulu kwa kupata alama nzuri.

“Huyu mwanafunzi tulimsimamisha na hakufanya mitihani, lakini matokeo yake yanaonekana amepata hivi; Civics D, Historia D, Jiografia C, Kiswahili D, English C, Physics D, Chemistry C, Biology C, Basic Mathematics D, ambapo amepata daraja la tatu pointi 24,” alisema Bujugo.

Alimtaja mwanafunzi mwingine, Martin Rushaigwa, namba 01197/0173, ambaye alifanya masomo ya ‘Arts’.
Alisema matokeo ya mwanafunzi huyo yanaonesha kuwa ameongezewa alama za masomo ya biashara ya Bookeeping na Commerce, ambayo hakuyafanya kabisa.

Alimtaja mwanafunzi mwingine aliyefanya mtihani huo lakini matokeo yake yanaonesha amewekewa ‘absent’ na mwanafunzi mwingine, Mbazi Volta, hakufanya mitihani lakini amepewa alama za ufaulu.

“Matokeo hayo yananipa wasiwasi kwamba yanaweza kuwa yamechakachuliwa,” alisema Bujugo.

Mkurugenzi huyo anaiomba Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kurudia kusahihisha mitihani hiyo ili kuondoa ukungu ulioligubika taifa kwa sasa kuhusu matokeo ya kidato cha nne.

Naomba usahihishaji urudiwe, maana huu ni ubabaishaji mkubwa…matokeo hayo yamewaathiri watoto kisaikolojia na sijui watakwenda wapi?,” alihoji.

Alisisitiza kuwa usahihishaji urudiwe kwani katika shule hiyo wanafunzi wenye uwezo mkubwa tangu walipoanza kidato cha kwanza ndio waliofanya vibaya wakati waliokuwa wakifanya vibaya, wameibuka na alama za juu.

Mkurugenzi huyo alisema wazazi wa watoto hao wanatarajiwa kukutana mwishoni mwa wiki hii kujadiliana kuhusu matokeo hayo na hatua za kuchukua.
Akitolea ufafanuzi suala hilo, Msemaji wa Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA), John Nchimbi, alisema si kweli kuwa matokeo hayo yamechakachuliwa bali ni matokeo halisi ya shule hiyo.

Alisema iwapo mkurugenzi wa shule hiyo ana shaka na matokeo hayo, alitakiwa kufika katika ofisi za baraza hilo ili apatiwe taarifa sahihi kabla ya kutoa taarifa katika vyombo vya habari.

“Mi nimeangalia hayo majina, naona yapo sawa na hata huyo mwanafunzi ambaye anasemekana hakufanya mitihani na akapewa alama…napenda kusema kuwa alama alizopewa si zake na hata katika orodha yetu anaonekana kuwa hakufanya mitihani,” alisema.

Katika hatua nyingine, Waziri wa wizara hiyo, Dk. Shukuru Kawambwa na wenzake, wamekuwa bubu kueleza endapo wako tayari kujiuzulu au la.

Tanzania Daima ilifika wizarani hapo jana kutaka kuonana na Waziri Kawambwa ili atoe msimamo wake, mwandishi alijibiwa kuwa waziri huyo alikuwa kikaoni na asingeweza kutoka.

Hata waziri alipopigiwa simu pamoja na kutumiwa ujumbe mfupi wa maneno, hakupokea wala kujibu ujumbe huo.
Kwa upande wake, katibu mkuu wa wizara hiyo naye hakuwa tayari kuzungumzia suala hilo kwa madai kuwa alikuwa kikaoni.

Naye Naibu Waziri, Philipo Mulugo, alipotafutwa kupitia simu yake ya mkononi kueleza msimamo wake, simu yake iliita bila kupokewa na hata hakuwa tayari kujibu meseji ya ujumbe mfupi.

50 Cent And Fat Joe Collaboration On The Way

50 Cent and Fat Joe were two of the rap dudes with the most beef in a minute. That wasn’t no Frank Ocean / Chris Brown mess. These dudes were going at it, if they  were to ever meet. But, they made up last year in light of the death of Chris Lighty. Now, the beef may officially be done. These dudes are rumored to be collaborating soon.
I think these rumors started with an interview 50 did. I wouldn’t bet on it though.

Download New Track!!! Dayna Ft Mr Blue-Leo


PICHA KADHAA YALIYOJIRI KWENYE BIRTDAY BASH YA BIRDMAN ILIYOFANYIKA 16 FEBRUARY





[PICHA] KILINGE CHA HIPHOP NA TAMADUNI MUZIK JUMAMOSI 16 FEBRUARY























RIHANNA NA CHRIS BROWN WAMEGOMBANA TENA MARA HII CHANZO KIKIIWA NI RAPPER DRAKE


Chris brown na Rihanna ambao hivi karibuni walirudiana rasmi na kudhihirisha hilo walionekana wakiwa pamoja kwenye tuzo za muziki za grammy,ila muda mfupi baada ya kutoka kwenye tuzo hizo couples hap wawili walionekana si wenye furaha na baadae kila mmoja aliondoka kivyake kwenye ukumbi huo.Ila chanzo kinasema chriss alimfuma rihanna akiwa anamtumia meseji boyfriend wake wa zamani Drake kitu ambacho kilionekana kumkera sana chris brown ambae ana uhasama mkubwa sana na drake

Tuesday, February 19, 2013

Download New!! [AUDIO] P The Mc-Huna Jipya


Download [AUDIO] JB Love-Me Na Hustle


Download [AUDIO] Mimu The Big Brother-MIMU (Produced By Duke Touchez)


Monday, February 18, 2013

UTARATIBU WA JINSI UNAVYOWEZA KUNUNUA NYIMBO MPYA YA P THE MC

 P The Mc anatimiza idadi ya wasanii 4 kutoka TAMADUNIMUZIK lebo ambao wameamua kutumia njia ya kuuza nyimbo zao moja moja kama njia ya kuongeza kipato kupitia mziki wanaoufanya,wasanii wenzake ambao wameshawahi kutumia utaratibu huu ni Nash Mc,Songa, na One The Incredibl.Feel at home km kawaida yetu tunakupatia utaratibu rasmi wa jinsi ambavyo unaweza kujipatia nyimbo hii mpya ya P The Mc ambayo inaitwa P Mawenge.Utaratibu ni huu "Unatuma sh 1000 kwenda namba 0717254451 (TIGO PESA) NA (M PESA) NI 0758033291.Tuma namba yako au e mail km unatumia whats up.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...