Thursday, May 31, 2012

DUDE: ALIYEIROGA BONGO MOVIES AMEKUFA

                                                           Kulwa Kikumba ‘Dude’

Na Erick Evarist

MSANII Kulwa Kikumba ‘Dude’ ameweka ‘plain’ kuwa kitendo cha wasanii wenzake (Bongo Movies Club) kumtenga amekifananisha na tasnia hiyo ya filamu kurogwa na mtu ambaye ameshafariki.
Akifafanua kauli yake hiyo, Dude alisema wasanii wameshindwa kuelewa kuwa wanapaswa kukanyana wenyewe kwa wenyewe lakini anapofanya hivyo wanafikia hatua ya kumtenga.
“Tunashindwa kuitumia fursa ya rais wetu anayependa sanaa kwa sasa, badala yake tunafanya mambo ya ajabu ambayo kimsingi yanatudhalilisha kwa jamii.
“Hatujui rais ajaye atapenda nini, kama akipenda uvuvi si itakuwa imekula kwetu...sasa wasanii ukiwakumbusha wabadilike, wao wanakuona adui,” alisema Dude.
Hivi karibuni ilidaiwa kuwa Dude ametengwa na Club ya Bongo Movies baada ya staa huyo kufanya mahojiano na Kituo cha Runinga cha Clouds na kuwaonya wenzake juu ya mwenendo wa kitabia.

 www.globalpublisher.com
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...