Thursday, August 2, 2012

MAKAMU WA RAIS DKT GHARIB BILAL AFUTURISHA MIGOMBANI UNGUJA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akijumuika na waumini wa dini ya Kiislam, katika swala ya Magharibi wakati alipojumuika na waumini hao katika Futari ya pamoja aliyowaandalia na kufuturu nao Migombani Unguja mjini Zanzibar jana Agosti 01, 2012.










Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya Waumini wA dini ya Kiislam, baada ya kufuturu nao futari ya pamoja aliyowaandalia Migombani Unguja mjini Zanzibar jana, Agosti 01, 2012. 
 Wake wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Zakhia Bilal (wa pili kulia) na Mama Asha Bilal (katikati) wakijumuika na waumini wa dini ya Kiislam, wakati wa futari ya pamoja iliyoandaliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, kwa waumini hao iliyofanyika Migombani Unguja, mjini Zanzibar jana Agosti 01, 2012. 
  Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal, akipiga picha ya pamoja na baadhi ya kinamama, baada ya kushiriki nao katika futari ya pamoja iliyoandaliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, iliyofanyika jana Migombani Unguja mjini Zanzibar
Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Zakhia Bilal, akipiga picha ya pamoja na baadhi ya kinamama, baada ya kushiriki nao katika futari ya pamoja iliyoandaliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, iliyofanyika jana Migombani Unguja mjini Zanzibar. Picha na Muhidin Sufiani-Ofisi ya Makamu wa Rais
 
 Habari kwa hisani ya www.hakingowi.com
 
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...