Thursday, August 2, 2012

Rais wa Zanzibar Dk Ali Shein Atua Kusini Pemba na Kufuturisha

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Ahaj Dk.Ali Mohamed Shein,na Mkewe Mama Mwanamwema Shein,wakiagana na Viongozi wa Mikoa ya Pemba katika Uwanja wa Ndege wa Karume Pemba,baada ya kumaliza Ziara ya kisiwani humo.
   Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,(kushoto) akisalimiana na Viongozi na wananchi wa Mkoa wa Kusini Pemba alipowasili katika viwanja vya Skuli ya Mkanyageni Pemba katika chakula cha Futari aliyowaandalia wananchi na waumini Kijiji cha Mkanyageni katika mwezi Mtukufu wa Ramadhan jana. 
 Sheikh Yussuf Abdalla,wa Kijiji cha Mkanyageni Wilaya ya Mkoani Pemba akitoa shukurani kwa niaba ya wananchi wa kijiji hicho kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Moahmed Shein,kwa kuwaandalia Chakula cha Futari,iliyofanyika jana katika Viwanja vya Skuli ya Mkanyageni Mkoa wa Kusini Pemba.
   Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,(wa pili kulia) akijumuika na wananchi wa Kijiji cha Mkanyageni Wilaya ya Mkoani,Mkoa wa Kusini Pemba,katika chakula cha Futari,aliyowaandalia Wananchi hao katika viwanja vya Skuli ya Mkanyageni
 Baadhi ya akina mama wa Kijiji cha Mkanyageni Mkoa wa Kusini Pemba wakiwa katika chakula cha Futari katika Mwezi mtukufu wa Ramadhan,iliyoandaliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,katika viwanja vya Skuli ya Mkanyageni Pemba   
 Baadhi ya Wananchi na waumini wa Dini ya Kiislamu wa Kijiji cha Mkanyageni Mkoa wa Kusini Pemba wakiwa katika chakula cha Futari katika Mwezi mtukufu wa Ramadhan,iliyoandaliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,katika viwanja vya Skuli ya Mkanyageni Pemba

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,(wa pili kushoto) akiagana na Wananchi wa Kijiji cha Mkanyageni Mkoa wa Kusini Pemba jana baada ya Chakula cha Futari aliyowaandalia katika viwanja vya Skuli ya Mkanyageni.Picha na Ramadhan Othman,Ikulu-Zanzibar
 
habari kwa hisani ya hakingowi.com
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...