Saturday, August 4, 2012

KILICHOMUONDOA 'ASHA NGEDELE' ORIJINO KOMEDI HIKI HAPA


UKISTAAJABU ya Mussa Hutayaona ya firauni,msemo huo umetimia hivi karibuni mkoani hapa baada ya mawaziri,wakuu wa mikoa na familiya ya Mzee Ngedele,kumpiga marufuku Mpoki kumzal ilisha dada yake wa damu Asha Ngedele kwenye vipindi vya kundi la vichekesho la Orijino Komedi.
Hali hiyo imebainika hivi karibuni baada ya familia ya Ukoo wa Ngedele kuwapiga marufuku kundi la Orijino komedy kulitaja jina la ukoo huo wa marehemu Ramadhani Ngedele wenye maskani yake maeneo ya Mji Mpya mkoani hapa. Kwa kipindi kirefu sasa baada ya kupigwa mkwala huo kundi hilo la Orijino komedy linalorusha michezo yake kila siki za alhamis kwenye luninga ya taifa ya TBC I baada ya kupigwa mkwara huo wamenywea na kukitoa kipengele hicho walichokuwa wamekipa jina la timbwili la Asha Ngedele.

Chanzo chetu cha habari cha kuamini kilidai kwamba takribani wiki mbili zilizopita familia hiyo ya Ngedele alimuita Asha Ngedele anayeishi jijini Dar es salaam kuja kwenye kikao cha familia kilichofanyika nyumbani kwao maaneo ya Mji Mpya,inadaiwa kwamba angendakuku ya kikao hicho ni kuhusina na Asha Ngedele kukubali kaka yake Mpoki kulizalilisha jina la ukoo huo wa Ngedele Mpoki na Asha Ngedele ni mtu na kaka yake wa damu ambapo Mpoki mama yake ni mdogo na Asha mama yake ni mkubwa, wazazi wao hao ni mtu na dada yake wa baba mmoja mama mmoja ambao kabila lao ni wapogolo wa lfakara wakitokea kwenye ukoo wa Kiwanga. Baada ya kupokea habari hizo mwandishi wetu aliingia kazini na kuwasaka wahusika wote ambapo wakwanza kupatikana alikuwani Mzee Msafiri Ramadhan Ngedele ambaye ni baba mdogo wa Asha alipohojiwa alisema,
“Nikweli sisi familia ya Ngedele tumezuia jina la ukoo wetu tuchafuliwa na kundi lile la Orijino Komedy mbaya zaidi na kinacho washangaza watu wengi ni kwamba Asha na Mpoki ni mtu na dada yake wa damu,hivyo ukoo tuliamua kuwapiga marufuku kulitaja jina la ukoo wetu pia jambo hilo lilikuwalikiwachukiza wajomba wa Asha na Mpoki ambao ni Waziri mstaafu Juma Ngasongwa na mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu hawa wanazaliwa na mama zao mama yake Asha ni mkubwa na mama yake mpoki ni mdogo"alisema mzee Msafiri Ngedele.
Alipotakiwa kuzungumzia jambo hilo mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu alisema kwamb ni kweli Asha Ngedele na Mpoki ni watoto wa dada zake na kwamba jambo hilo binafis lilikuwa likimchefua. "Mimi binafsi sijapata muda wa kukutana na hao wajomba zangu wakuzungumzana nao juu ya jambo hilo,lakini kabla ya kwenda kwa dada zangui ifakara nitakwedan kwa ukoo wa Ngedele kuzungumza nao tuangalie namna ya kuliweka sawa jambo hilo'"alisema Mwambunga ambaye kabla ya kuteuliwa kuwa mkuu wa mkoa,alikuwa ni mkuu wa Wilaya ya Morogoro.
Mtandao huu alipofika nyumbani kwa Waziri mstaafu DktJuma Ngasongwa maene ya Riti jirani na ofisi ya mkuu wa mkoa wa Morogoro kwa lengo la kusikia kauli yake juu ya jambo hilo alielezwa kwamba waziri huyo wa awamu ya tatu amesafiri. Kwa upende wake Asha Ngedele alipohojiwa kuhusiana na sakata hilo alidai kwamba kwake hakuna tataizo lolote na kwamba alilidhia jina lake kuchafuliwa'
"Kwa mtu mwenyeakili awezi kuchukua mambo ya kichezo ya kuingia na kaumjaji mtu kwamba ndio alivyo,ni kweli mimi mwenyewe nimelidhia kaka yangu kulitumia jina langu kwenye kundi lao"alisema Asha ambaye makazi yake yako jijini Dar es salaam
Mpoki alipohojiwa na mwandishi wetu kwa kupia simu yake ya kiganyani namba 0713 44 12## ambapo baada ya kusomewa tuhuma hizo alijibu kwa mkato akisema" Siko tayari kuhojiwa kwa sasa na " na kukata simu Ikumbukwe kwamba Asha Ngedele upande wa mama ni mpogolo na upande wa baba ni mrugulu,ambapo Mpoki pia upande wa mama ni Mpogolo na upande wa baba ni Mhaya Kwenye baadhi ya michezo ya kundi hilo la Orijino komedi Mpoki alisikika akimnanda dada yake huyo kwa kusema
'' We humjuia Asha Ngedele kabla ya kuja huku Dar alikuwa akijiuza pale Kahumba na kwamba alikuwa hana ukimnunulia supu ya mguu wa ng'ombe'Kongoro' unaondoka naye"
Athumani Ngedele ambye ni mdogo wake Asha alipohojiwa jana alisema kwamba kama familia walikuwa wakipata shida sana wanapojitambulsikwa jina la Ngedele" kwa mfano nikienda hospital nikitaja jina langu la Athumani Mohamed Ramadhan Ngedele watu wote waliokuwa eneo hilo wageuza shingo na kunitazama huku wengine wakiniuliza yule mwanamke kati Asha Ngedele ni ngugu yako,sio sili kunawaktia mwingine naladhimika kumkana dada yangu wa damu ambaye tumechangia baba"alisema Athuman
Mzee Msafiri Ramandhan Ngedele ambaye ndiye mkuu wa familia ya ukoo wa Ngedele baada ya ndugu zake kutangulia mbele za haki akiwemo baba mzazi wa Asha mzee Mohamed Ramadhni Ngedele.
Mzee Msafiri ambaye ni baba mdogo wa Asha ndiye aliyesima
ma kidete kulipiga marufuku kundi la Orijino komedi kulitumia jina la Ngedele kwa madai kwamba kundi hilo lilitumia jina hilo vibaya na kuzalilisha ukoo huo wa Ngedele wenye maskani yake maeneo ya Mji Mpya mkoani Morogoro.

Maneno Mohamed Ramadhan Ngedele ambaye ni bingwa wa kusakata disko Afirika mashariki na kati aliyetapa kwenye fani hiyo miaka ya 90 akionyesha umahiri wakwe hivi karibuni ndani ya ukumbi wa DDC mkoani Morogororo.
 
 STORI NA  DISMAS TEN KWA MSAADA WA  BONGO DAWN TOWN
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...