Monday, August 8, 2011

WAKENYA WANAOKABILIWA NA NJAA, WAHAKIKISHIWA KUPATA CHAKULA



















Katibu mkuu wa shirika la msalaba mwekundu nchini Kenya, Abbas Gullet, anawahakikishia wakenya wote wanaokabiliwa na njaa kwamba msaada wa chakula uliotolewa na mpango wa Kenyans for Kenya, utagawanywa bila mapendeleo.  Akiongea mapema leo katika afisi za shirika hilo, gullet amesema awamu ya pili ya kusambaza chakula hicho cha msaada itatekelezwa katika maeneo ambako chakula cha msaada hakijafika. Wakati huo huo, wanaharakati wa kundi la unga revolution, wanaopigania kupunguzwa kwa gharama ya maisha, wanawataka Rais Mwai Kibaki na Waziri mkuu Raila Odinga kuchukuwa hatua za kupunguza bei za vyakula nchini.

0 comments:

Post a Comment

CHANGIA MAWAZO YAKO HAPA

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...