Sunday, July 24, 2011

Hammam kukata rufaa

Aliyekuwa rais wa shirikisho la mchezo wa soka barani Asia, Mohamed Bin Hammam, anatarajiwa kukata rufaa dhidi ya marufuku ya maisha ya kutoshiriki katika shughuli zozote za mchezo huo, aliyopewa na shirikisho la mchezo wa soka duniani FIFA.
                     Aliyekuwa rais wa shirikisho la mchezo wa soka barani Asia, Mohammed Bin Hammam

Bin Hammam ambaye anatoka Qatar, alipewa hukumu hiyo kufuatia tuhuma za kununua kura wakati wa uchaguzi wa urais wa FIFA ambao alikuwa mmoja wa wagombea wa kiti cha urais.
Katika mtandao wake, Bin Hammam, ametaja matukio ya hivi karibuni kama mapambano katika vita vinavyoendelea.
Vile vile amechapisha barua inayopongeza juhudi zake, katika shirikisho hilo iliyoandikwa mwaka wa 2008 na rais wa FIFA, Sepp Blatter.
Chini ya barua hiyo kuna mstari unaosema "Hii ni mapambano na sio vita vyenyewe".

0 comments:

Post a Comment

CHANGIA MAWAZO YAKO HAPA

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...