Thursday, June 16, 2011

Zawahiri sasa ni mkuu wa Al-Qaeda

Ayman al-Zawahiri, ambaye kwa muda mrefu mno amekuwa msaidizi wa Osama Bin Laden katika kuiongoza Al-Qaeda, na akishikilia nafasi ya pili katika kutoa amri, sasa ataliongoza kundi hilo.
Hayo ni kwa mujibu wa taarifa katika wavuti ya kundi hilo.

Bin Laden aliuawa nchini Pakistan alipopigwa risasi na kikosi maalum kutoka nchini Marekani mwezi Mei.

Kundi la Al-Qaeda limeonya kwamba litaendelea na vita vyake dhidi ya Marekani na Israel chini ya uongozi wa Zawahiri.

Wadadisi wa masuala ya Al-Qaeda wanaelezea kwamba Zawahiri, mwenye umri wa miaka 59, na aliyezaliwa nchini Misri, ni mtu mwerevu sana, lakini hana uwezo wa kuwavutia wafuasi wengi kama alivyofanya Osama.

Baadhi ya wadadisi wanasema yeye ndiye aliyepanga na kuendesha shughuli nyingi zilizohusiana na shambulio la Marekani la 9/11.

Kwa muda wa miaka mingi, msaidizi wa Bin Laden, ambaye atakayefanikiwa kumpata atapokea dola milioni 25 (pauni milioni 15), alitazamiwa kurithi madaraka hayo.

Taarifa iliyotangaza madaraka hayo ilichapishwa katika wavuti ya Al-Qaeda, na kusemekana imetolewa na uongozi wa juu unaotoa amri katika kundi hilo.

"Sheikh Dk Ayman al-Awahiri, Mungu amsaidie, katika kuendelea na uongozi wa kundi", taarifa ilielezea.

Taarifa ilielezea kwamba chini ya Zawahiri, itaendelea na vita vitakatifu vya Jihad dhid ya Marekani na Israel, "hadi majeshi yote ya wavamizi yanaondoka kutoka ardhi ya Waislamu".

0 comments:

Post a Comment

CHANGIA MAWAZO YAKO HAPA

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...